Jumatano, 19 Desemba 2018

FOURTHFALSEWORLD

FOURTHFALSEWORLD
DUNIA YA NNE YA UONGO
Kila mmiliki wa mtandao wa kijamii akihojiwa nini nia na dhumuni la kuanzisha mtandao wa kijamii? huwa anasema ni kwa ajili ya kuwaleta watu pamoja.
Swali ni je umeletwa pamoja au umeletewa hoja ya uongo ya pamoja?

Lakini swali hilohilo tukiulizana watumiaji je tumeletwa pamoja kweli? nadhani majibu yatatofautiana right?

Labda mimi nianze kwa upande wangu kutokana na experience yangu ya kutumia mitandao ya kijamii kwa muda mrefu sasa.

Ukiniuliza mimi sasa nitakujibu kama ifuatavyo tena kwa ufupi tu maana kwa urefu hatutomaliza leo.

MAJIBU:-
Nauona umoja wa uongo katika dunia hii ya nne ya uongo,naona maisha yetu ya uongo ndani ya dunia hii ya uongo,naona kundi langu la uongo la marafiki 4000 na ushee waliombatana na mimi kiuongo pia najiona mimi ni miongoni mwa rafiki wa uongo kwa baadhi ya marafiki zangu ambao wanaendekeza uongo katika ulimwengu huu uliojitenga na uhalisia,Naona picha nasioni maelezo ya kweli juu ya uhalisia kwahiyo nao ni uongo pia,naziona video za utupu na kufuru mtandaoni kitu ambacho sikioni mitaani kila nikijaribu kupeleleza ili nikiweke sawa,nawaona marafiki zangu wakiwa kwenye mahotel makubwa,majumba ya kifahari na magari ya kisasa na wengine kwenye ndege kabisa lakini nikikutana nao nakumbuka kuwa sharti la dunia ya nne ni lazima usiishi kama unavyoishi dunia ya tatu so? ni uongo pia au?,
Nawaona marafiki wanaotuma picha wanakula vyakula vya ghali na nikigeukia majumbani mwao nasikia kelele za wadogo zao wakigombaniana nani ale kichwa nani ale mkia,Nayaona mapenzi ya dhati mtandaoni wapenzi wanapokutana katika dunia hii na siioni furaha yao katika uhalisia,Nayaona mapenzi ya uongo pia yanayoanzishwa na kufia hukuhuku katika ulimwengu wa uongo bila ya watu kukutana na mmojawapo tayari keshatapeliwa,Nawaona marafiki wanaotuma picha wakiwa wamevalia nguo mpya kila siku mtandaoni na tukikutana uraiani nakumbuka walikuwa wakifanya biashara za marafiki zao wenye camera na maduka ya nguo,naonana na ndugu na jamaa kila siku nikiingia katika ulimwengu huu na tukikutana husema aidha wamenisahau au hata wanaonikumbuka huniuliza mbona huonekani siku hizi? umekuwa adimu best..!! nikakumbuka kumbe ninaedit sana picha kuonekana nimeng'aa kumbe nimepaushwa na dhiki na baridi la njombe,naona picha za watu waliofariki wakapostiwa na ndugu zao wa karibu bila ya kuombwa ridhaa zao pindi walivyokuwa hai na watoa maoni hutoa maoni yao kwa kutetema na kuhuzunika kwa kuandika RIP na wengine jinsi walivyo waongo zaidi hulike vifo hivyo huku wao binafsi wanaogopa kufa sasa najiuliza wanalike nini?,Naliona kundi la watu lililojitenga na uhalisia na kuishi ndani ya mfumo wa dunia ya uongo na hata kubadili majina yao kujiita majina ya kike na wanawake kujiita ya kiume kwasababu wanazozijua wao wenyewe binafsi,Nawaona waandishi wenzangu tunaojitahidi kuielimisha na kuihamasisha jamii kila siku na bado dunia hii na watu wake inatupiga vita tusivifikie vizazi vyao zaidi,Nawaona ndugu jamaa na marafiki ambao wanaongea zaidi kiingereza mtandaoni huku uraiani ukiwasalimia tu hawataki kukujibu kwa lugha ya kiingereza wanayoiongea katika ulimwenguni huu,bado nawaona wakituma picha wakiwa wameonesha sehemu za nyuma za miili yao huku wakiwa wamevaliwa mavazi ya ajabu kwa ajili ya comments,followers,likes,viewers,shares n.k huku nikigeuka ulimwengu wa tatu muda wote wana vitenge maungoni,Naziona ajali nyingi katika ulimwengu wa tatu zinazosababishwa na madereva ambao huendesha vyombo vya moto huku wakiwa ulimwengu wa nne,Nawaona wanaharakati wanaokemea maovu kwa kupaza sauti wakiwa ulimwengu wa nne na wakirudi ulimwengu wa tatu huambatana na maovu wanayoyakemea,Nayaona madarasa mengi na sioni walimu katika ulimwengu huu,nawaona madaktari na sizioni tiba,nawaona mafundi na sipati huduma stahiki,naziona bidhaa na biashara nyingi za kupendeza katika ulimwengu huu lakini nikizinunua hazifanani na wakati mwingine sizipati kabisa,naziona ripoti na takwimu za uongo ambazo kila siku zinasambazwa na kuvifanya vizazi vya kutafuniwa viamini katika uzushi,Naziona  chuki na wivu vikishamili ndani ya ulimwengu huu wa nne kutokana na uongo uliopo ndani yake,tambua naona pia kuna ubaguzi na unafiki katika mengi yatendekayo katika ulimwengu huu wa nne wa uongo.

ULIMWENGU WA NNE WA UONGO NI KAMA BLANKET NZITO KWA WAAFRIKA NA WAJINGA WOTE ULIMWENGUNI.
Wanasema aliyelala usimuamshe kwani akiamka utalala wewe je unaujua upande wa pili wa msemo huo? uko hivi:-
aliyelala usimuamshe bali muongezee joto.
Jamii zetu za kiafrika zinasubiri birthdays kwa hamu na shauku kubwa kuliko tunavyomsubiri Masihi na ukombozi kabla ya siku ya kiama.
Walianza taratibu kutujaribu kwa masuala ya sikukuu za kipuuzi eti ili kufurahi mwagianeni maji walivyoona tumekubali wakatuletea mfumo wa matope ili tuzidi kuingiza matope zaidi vichwani mwetu hiyo bado haikutosha na sisi kwa fikra zetu zilizojaa matope tukaamua tumwagiane hadi oil chafu bila kujali athari zake nadhani mpango ujao tutapakana vinyesi kabisa by the way you have to be ready fools the plan is coming soon.
Kula keki tu haikutosha katika hayo masikukuu yetu yasiyowajumuisha hata wazazi/walezi wetu waliofanya juhudi za kutuleta hapa duniani na kutulea kinyume chake tunawaalika marafiki zetu tuliokutana nao tukiwa na meno 32 na twafanya sherehe mahali paovu na matendo yamchukizayo Mwenyezi Mungu.
Can I ask a question?
kiburi hiki cha uhai tunakitoa wapi? okay tuendelee tulipoishia.
.......tukaona haitoshi na tukaamua kuanza kubandikana keki usoni huku baadhi ya sehemu kama somalia,yemen,congo,afrika ya kati,sudan n.k kuna watu wakiwemo wazee,wanawake na watoto wanakufa na njaa.
Jamii yetu imekuwa ikiguswa sana na kupiga makelele juu ya maswahibu yanayokuwa yanawakumba watu maarufu kuliko kuweka juhudi katika kuzipigania familia zetu zitoke katika tabaka lililopo hivi sasa yaani tuliurithi ujinga,tunauishi ujinga,tunauendekeza ujinga na kuvirithisha vizazi vyetu ujinga pia
Hivi yule Tanasha wa diamond anatuingizia shilingi ngapi tunavyomnanga mitandaoni eti nyuma kapigwa pasi niulize hivi kwani mlitaka apigwe nini? passport?
Haya leo diamond na Rayvanny kafungiwa kwani wewe mbona umejifungia mafanikio yako na baraza la ujinga na wala hupigi kelele wala kukata rufaa kwa kuyafuata maarifa?
Darassa alikuwa anakula madawa ya kulevya na amerudi akiwa hana hata dalili ya uteja ndani yake vipi unajisikiaje mwafrika mwenzangu hivi ilikulipa nayo hii?
#BringBackOurMo  yeah alirudi and then? mana sisi tulimuita OurMo sijawahi kumsikia akituita My everythingTanzanians.
Tunasifika kwa ukarimu sikatai
Na tukumbuke tunasifika kwa unafiki na uvivu pia upo?
#2019TUACHEUJINGA

Mpango wa manguruwe nyie mnawaita wahisani au wazungu I don't know what the hell are they.
Sio tu kuwafanya mpungue bali na wachache mnaosalia muwe wajinga ukiisoma na kuichimba vizuri historia ya mtu mweusi hutokaa kujikenusha ukimuona mzungu au kujitia mwema mbele ya hawa watu weupe kwa ujumla mana hata wachina,wahindi,na waarabu ni washenzi pia vilevile.
Kati ya watu wenye akili ulimwenguni basi mtu mweusi anastahili kuwa nambari moja kabla ya warusi na waisrael.
Je unaijua historia ya Saa ilianzia wapi? Afrika(Misri) Je Mansa Mussa alikuwa anatokea wapi vile? Afrika(Mali).
Kwani nassa walivyokuwa wanataka kurusha chombo chao kwa mara ya kwanza mwezini walikuwa wanafeli wapi mpaka kikawa kinafeli? unajua ni nani aliyekuja kukiwezesha kiruke? ni yule mama mweusi waliyekuwa wanambagua kisa ana asili ya afrika.
Hivi unamjua Christopher Columbus kweli? Je wakina Martin Luther,Malcom X,Mandela,Nyerere n.k
Je unahitaji reference zaidi? learn to use your brain strictly my friend.

Mitandao ya kijamii naitafsiri kama blanket nzito kutokana na namna akili za vijana wengi kuwa za mfanano na zenye kugubikwa na fikra mgando kutokana na kufurahia maisha fake ya ulimwengu wa nne.
Blanket hili limetupelekea kujiona hatuwezi kuyaendesha maisha kwa usahihi bila ya uongo uongo ndani yake.
Blanket hili limetufanya kuwa wavivu na watumwa kila kukicha.

Kama umelala na hauamshwi kuiona dunia inavyokwenda kasi basi nimeamua kukuamsha kwa kukupa kahawa lita mbili,energy katoni moja na njaa isiyokoma ili usilale tena.
Ila ni maamuzi yako pia kuishi katika ulimwengu wa tatu kwa fikra za ulimwengu wa nne.

BY THE WAY NIWASHUKURUNI SANA KWA KUWA SEHEMU YA KUELIMIKA NA MAARIFA HAYA MUNGU AWABARIKI SANA NA MUWE NA SIKU NJEMA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni