Jumapili, 23 Juni 2019

KAMA ningali
Kama ningali rejea utotoni basi nisingelifanya utoto ningali mtoto.

Mambo mengi ambayo huwa yanakuwa yanaanza kuonekana yanakwenda kombo huwa tunayaficha nyuma ya kauli "KAMA ningali" ili kuonesha na kudhihirisha dhahiri kwamba ni kweli tumesukumwa na hali fulani kushindwa kulitimiza jambo fulani.

KISA CHA KIJANA
Kijana mmoja mtanashati anayeishi katika nyumba ya wazazi wake iliyo nzuri ndani na nje ikiwa ina bustani ya kupumzikia na ina eneo kubwa linalowezekana kufugia mifugo midogomidogo.
Kijana huyu ana elimu ya chuo kikuu na alitunukiwa shahada ya utawala wa biashara huko chuoni CBE Dar es Salaam barabara ya bibi titi mohamed kijana alizawadiwa zawadi kemkem wakati akihitimu na moja ya zawadi hizo ilikuwa ni simu ya rununu tanashati aina ya Samsung Galaxy S9 ya mwezi machi mwaka 2018 toleo la kwanza inayogharimu kiasi cha shilingi milioni 2,300,000/= za kitanzania.
Kijana anamiliki wapenzi wanne watatu ndani ya mkoa na mmoja yupo nje ya mkoa na wote anawasiliana nao kwa pesa ya vocha kutoka kwa baba yake anazompatia kama nauli na vocha pindi aendapo kutafuta kazi baba yake ni mtumishi wa halmashauri.

Lakini kjana anatamani sana kuianzisha biashara yake kwani ana elimu nzuri ya biashara lakini kijana kila siku husema "KAMA NINGALIKUWA NA MTAJI BASI NINGALIANZISHA BIASHARA YANGU."
JE KIJANA ANAHITAJI MTAJI WA NINI ILI AANZE KUFANYA BIASHARA?

Kama ningali na-jua ningeliishi sayari ya peke yangu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni